MAONESHO YA BIASHARA YA KIMATAIFA KWA A. MASHARIKI
Na Mjomba Remsi
Dar Es Salaam, 14 July 2016
Maonesho ya Biashara ya Kimatifa – International Trade Exhibition
yaliyodumu kwa siku mbili yamefikia ukomo leo, baada ya washiriki wa kimataifa kuonesha bidhaa zao na
vifaa vyao wakiwa wamelenga nchi tano (5) za Afrika ya Mashariki.
Maonesho hayo ya biashara
yalikuwa na bidhaa mbali mbali zikiwa ni vifaa vya viwandani na vifaa vya kilimo na madawa pamoja na
mawasiliano – teknohama.
Mabara matatu yaliwakilishwa kwa
uwazi kabisa ikiwa ni pamoja na makampuni ya kutoka Bara la Ulaya, kutoka Asia
na Afrka. Hali kadhalika eneo la Eurasia lilipata uwakilishi katika maonesho
hayo ambayo yalikuwepo Mlimani City, kuanzia Julai 13.
Katika maeneo yaliyoweza
kuonekana kwa haraka haraka ni
vifaa vya viwandani kama vile
mashine za kutengenezea nyaya, mashine za kuchimba ardhi na kilimo-
earth moving and agricultural equipments pamoja na mmitambo ya kuchapisha
vitabu magazeti na vipeperushi.
Afrika Mashariki ina wakazi zaidi
ya milioni 100 wakiwa wanaishi katika nchi za Burundi, Kenya, Rwanda , Tanzania
na Uganda. Na Lugha kuu zinazotumika katika maeneo haya ni Kiswahili ambacho kitumika katika nchio zote
bila mipaka, Kingereza ambacho kimo kwa wingi katika nchi tatu zikiwa
ni Kenya Uganda na Tanzania na Rwanda kidogo. Halafu lugha ya Kifaransa ambayo
inatumika Burundi na Rwanda.
Wananchi wake wengi ni wakulima
na hivyo kwa makampuni yaliyoshiriki
katika maonesho kuandaa maonesho ya bidhaa za kilimo na namna ya kutengeneza na
kutayarisha mazao ndio hasa mahali pake.
Washiriki wengi ambao ni wageni
walifurahi sana na kusema kuwa wamepata wageni- wapitaji kuangalia bidhaa na
kuuliza na kuweka maandaliizi ya
mawasiliano pamoja na mikataba walikuwa
ni wengi.
Hata hivyo kuna makampuni mengine
ambayo yalikuwa yako tayari kuingia ubia na makampuni ya hapa Afrika
Mashariki au kwa uchache kama
wangelipata mawakala wao kwa bidhaa zao.
No comments:
Post a Comment