LOCATIONS



NZEGA,  FAST GROWING TOWN  AND SOON TO SURPASS TABORA

Mjomba Rems,

There was a time, when  somebody living anywhere in Nzega District, after the afternoon said, I want to go to town. People would ask him, By what means  or do you use a wungo? That was because mjini then was referred to Tabora only and every other place in the area was Kijijini and those intending to go to Nzega would refer to it as Wilayani.
After the mines and many developments in communications, now Nzega has boomed up. It needs to be a region  of its own as the town is so large  just as Tabora town was  30 years ago and the communications are better than what Tabora town had in that time.
Nzega is a hub of matters:
1.    It is a hub of business  as far as minerals are concerned, you have every thing from zinc, lead to gold. Nsungangwanda is part of it.
2.    In transport, Nzega is  not that backward. The tarmac stretches from Nzega to Mwanza and of course straight it goes through Ipuli to the Central Bus Stand  of Tabora at Kachoma.
3.    Political Hub as that is the place where we had great politicians of Tanganyika and Tanzania namely Kasella Bantu and others. Kasella Bantu is always remembered in his case  when he was the MP of the area and cattle rustlers  menaced the area and he  said, WINJAGI DOH!. ..meaning  only remove them.  And when the rustlers came again this time, the villagers came with a village call named MWANO and the whole village fell on them and  crushed them to pulp. The Mp was arrested in that case.
4.    Nzega is Historical as that is where the name Mwaisela Ward of Muhimbili  comes from  as there was a doctor of that name who lost his life at  Uchama area and he was a famous person not only then and even now.
5.    And on the other side Tabora seems to be at the dead end as the roads towards South are hazardous, there are  at signs along Sikonge Road that show that you travel on your own risk  as there is a sign of  a human skull and leg bones just like the flag of the PIRATES. 

SIKONGE
Cheupe Nyati,

     Katika majina ya maeneo ya Mkoani Tabora, mengi yamekosewa lakini la Sikonge limekosewa zaidi  na kuna haja ya kulisahihisha na kuleta usahihi wake  katika maandiko mbali na vitabu.



    Hayo yalisemwa na Mzee Mwana Kamwelwe, Ise wa Mbogo, akifafanua kuwa jina hilo usahihi wake ni VIKONGE, na hiyo ikiwa na maana ya mikonge ambayo kwa  jina jimgne ni katani.

    Mzee Mbogo ambaye anaishi maeneo mjini Sikonge  anasema mpaka hivi leo watu wakizungumza kwa Kinyamwezi hawatamki Sikonge bali, mtu anasema “Naya Vikonge “ maana yake “Nakwenda Vikonge”.

    Akielezea asili ya neno hilo alisema kuwa eneo la wilaya hiyo lina mimea hiyo ambayo Wanyamwezi wanaiita “makonge” na yako mengi. Yanapatikana karibu katika kila kisuguu.

“   Tangu zamani tulikuwa tukichukua mimea hiyo na kuichuna na kupata nyuzi zake ambazo ni nyeupe kabisa na tunasokota na kupata kamba kwa kazi nyingi tu”, alisema Mzee Mbogo.

    Akielezea kuwa akasema kuwa  kamba hizo zilitumika kusokota kamba nyembamba na kamba kubwa kabisakama ifuatavyo:

1.     Kapwe- ni kamba nyembamba ambazo hutumika kwa kutegea ndege  wadogo wadogo kuanzia jorowe, tetere (njiwa mwitu), huwa tutu (mapula), kwale na makanga.

2.     Ipwe- ni kamba ambayo ilitumika kwa mitego mikubwa  kwa ajili ya wanyama  wakiwemopaa, nyemela na  wanyama wengine wengine ambao umbo lao halizidi kimo cha mbuzi.

3.     Ngwisi – kamba ambayo ilitumika kufungia mbuzi, kondo na ng’ombe  wakati wa kuwakamua maziwa  ng’ombe anafungwa miguu yake na wakati wa kulima kamba hiyo inazungushwa kwenye pembe. Unene wa kamba hii Unaweza kuwa kama dole gumba au kama dole gumba la mguuni kulingana na haja ya kazi.

4.     Igalavwa  - Ni kamba ambayo unene  unazidi dole gumba la mguuni nampaka kuwa na ukubwa  wa mkono. Matumizi yake ni mengi sana lakini tusheke tu na kusema kuna matumizi ya:
a)     Kwa ajili ya shughuli za kutunduka na kushusha mizinga ya asali (nyuki).
b)    Hutumika kwa kazi za ujenzi na shughuli za kupasua mbao.

c)     Kamba kama hiyo ikitumika katika michezo ya kuvutana- Kavwivulule/Tug of war

                      


     Aina ya kamba iliyotengenezwa kwa kutumia nyuzio za katani ikiwa imetumika kwa kusuka kutumia minyororo mitatu. Aina nyingine ni kwa kusokota kwa kutumia minyororo miwili


Kwa kusisitiza kuwa jina hilo linatakiwa kubadilishwa  Mzee Mbogo alisema kuwa  hiyo katani iliyotoka huko  Marekani imetokea mahali panapo itwa Yukatan na hilo jina halikubadilika  kwa nini jina la VIKONGE libadilike, je ni kwa sababu watu wanashindwa kusema Vi au inashindwa kuandikika.  
Mbona Landani hawaiandiki wenyewe kuwa ni Landani wakati wanaandika ni London na  wanajua vipi wanatamka lakini na sisi  shauri zao watamke namna watakavyo lakini jina letu libaki Vikonge. Alisema kwa kusistiza.

 Akitaja neema za Wilayani Vikonge Mzee alisema kuwa  kulikuwa na Hospitali ambayo ilikuwa inajulikana nchi ya Tanganyika nzima na  ambayo ilikuwa pale mahali panaitwa Misioni, “Bado ipo. Lakini wapi Madaktari? Nani atamfikia Daktari akiitwa Kiveli? We acha tu.”  


Wilaya saba (7)  za mkoani Tabora na Wilaya ya Vikonge ikiwa katika rangi nyekundu
(ramani kwa hisani ya mtandao)



Aina ya Mkonge unaopatikana katika aina mbali mbali za mbuga za Sikonge/Vikonge

Ambazo sasa zinatengenezwa kama mauwa kwa ajili ya mapambo ya nyumbani. ( Picha na iita8860)


Aina nyengine ya mkonge ambao unapatikana katika nyika za Sikonge/Vikonge
Ikiwa Ndiyo mimea ambayo Ndiyo asili ya sehemu hiyo kuitwa Vikonge  kutokana na

Vikonge hivyo (picha kwa hisani ya internet)



No comments:

Post a Comment