Thursday, October 13, 2016

UKIWA KONGO USI JIUGUZE

 Na Cheupe Nyati   in Prague             

Katika mazungumzo na watu ambao wametembea hasa katika mipaka ya nchi za maziwa makuu.
Nchi ambayo inaogopwa sana ni Kongo. Kongo hakuna wizi, kongo hakuna utapeli, kongo  kuna mambo mengi sana.


Lakini kwa leo hii nakwambia kuwa nilipata habari wakati  nikisoma nje ya nchi – overseas, basi tulikuwa na kijiwe sisi watoto ambao tunaozungumza Kiswahili.
Walikuweko:
1.     Wakongo
2.     Warundi
3.     Wanyarwanda
4.     Wakenya
5.     Wabonngo
6.     Na  waganda

Katika visa vilivyokuwa vinatolewa  ilikuwa ni mtu anaweza kueleza ama yale aliyaona au yale ambayo anaona kuwa ndiyo mila na tabia za kwao.
Huyu mtu ambaye alikuwa ni Mkongo , lakini alikuwa na nyaraka za safari za Kibongo kamili kabisa. Alisema kuwa pamoja na kuwa pasi hiyo aliipata Tabora,  Tabora siyo asili yake bali yeye alitokeya Kivuu.
Anaeleza pamoja na mambo mengine yaliyokuwa si usalama kwake huko mpaka akakimbia akiwa na miaka kama saba au minane  ni kukwepa mauaji ya Pierre Mulele ya Mayimayi.

Kubwa zaidi ni kuwa yeye alikuwa amezaliwa pacha na mweziwe. Katika maisha yao kabla hata hawajaanza kwenda shule  alikuwa anaona  watu wanafanya mambo ambayo alikuwa hayaelewi. Mtu akiugua  basi kabla muda haujapita mrefu anasika kimya huyo mtu hayupo na wala watu hawasemi kitu juu yake.

Siku moja  akaona babu yake ambaye alikuwa anaitwa Muzee Mayuto ameletewa mzigo umefungwa na majani ya mugomba. Yeye aliwaambia wapeleke huo mzigo huko chumba cha ndani. Walipita na madamu yalikuwa yana vuja . Ah hao mabwana waliingi humo ndani na kutua mzigo wao wakatoka . Muzee Mayuto akauliza mzigo umetoka wapi huo? Wale watu wakasema Yule ni mutoto wa Muzee Kasembe kule kwa upande wa ng’ambo ya muto.  Muzee  Mayuto  akasema mbona gafla hivyo na alimuona kule kwenye arusi ya Kitwana  enga mbili zilizopita.  Ah weye muzee hizo ndizo salamu za Muzee Kasembe hawezi kukusahau wewe rafiki wake mpendwa. Boh
Inga ile ilipita na sisi tulikuwa tunafurahi kuwa na mchuzi mule kwetu. Lakini Yule ndugu wangu pacha alishikwa na homa kali sana  na akawa ana tetemeka. Mara wakaja wale watu walioleta salamu kutoka kwa Muzee kasembe  wakasema wanamuliza Muzee Mayuto, “Muzee Kasembe anauliza vipi  hakuna salamu zozote  maana kachoka kula ugali na sombe anataka apate kamchuzi kidogo.” Muzee Mayuto akasema apana hamuna kitu. Wale wajumbe wakasema mbona wamesikia  kuwa humo kwake mambo tayari  yeye anangoja tu , lakini usimusahau kamchuzi.. sisi tunakwenda “
Wale watu walikwenda na huku nyuma nikamuliza babu  kuwa wale walikuwa kina nani na walikuwa wanatafuta nini mbona salamu zao hazifahamiki…. Babu alicheka sana akasema , “Ah na weneye mguruguru sana  hebu tiondokeye hapa”.
Kwa kuwa ndugu yangu alikuwa yumo ndani  mimi nichukua manati yangu na kuingia msituni nikawinde ndege. Nilifika huko nikapotea njia  mpaka usiku ukaingia  na mara kwa bahati tu na mwezi ulikuwepo nikatokezea nyumbani.
Nikakuta watu wamekoka moto na wanaota hapo usiku, lakini palikuwa kimya  na hakuna mtu anayesema kitu. Mara nikaona watu wanatoka ndani na mizigo ya vitu vimefungwa kwa majani ya migomba , hao wanatoka na wanakwenda ; Walipotoka Muzee Mayuto akasema mupeni salamu zake Kasembe, lakini  kalikuwa bado kadogo aniwie radhi… tunaonana siku nyingine.
Ehe jamani  kumbe Yule pacha wangu amekwisha kufa na watu wamemchaanga na kupeleka zawadi kwa jamaa zake Muzee Mayuto. Lakini sisi mule ndani ni mwiko na mwiko kabisa kula muchuzi wa mtoto wa mule ndani.
Aa ah! Kumbe ! sana nifanye nini miye Mayuto mudogo… kimya kimya nilizunguka  nyuma ya nyumba na mwezi huo unang’aa nikaondoka nikaenda kutoka pale kijijini kwetu mpa nikafika Uvira. Muji wa Uvira siujui na sina mtu ninaye mujua pale , lakini watu walikuwa wengi tena wengi tu wanakwenda huko jua linakotoka wana sema kuna bahari lakini nyuma ya bahari kuna watu wazuri sana. Ah Bwana nilijiunga na watu hao wanaokimbia Mayi Mayi  namie namkimbia Mayuto , lakini jina langi ni Mayuto kama Babu.
Huko jama zangu katika kijiwe hicho niliwaambia hata jua likitoka magharibi kwenda Mashariki siwaambii kijiji changu najua kipo na watu wapo na wanajua kuwa walipotelewa na mtoto… najua wapo na huko sirudi  ntakwenda tabora na ntaka  Ulyankulu au Pangale.
Mtu huyo yupo hapa Tanzania  na anauwezo wa kuzungumza zaidi ya Lugha saba kwa ufasaha kabisa, lakini wewe muulize anaitwa nani  hapo utakuwa umezuwa ugomvi na ataondoka bila kuaga.
Hivyo ukiwa Kongo usivunge kuungua ….


No comments:

Post a Comment