Hali ya chama cha wananchi (CUF) kuwa katika hali
isiyoeleweka kunatia wasi wasi juu ya
uimara wa chama hicho kikiwa kama miongoni mwa vyama Vya upinzania vyenye nguvu
nchini Tanzania.
Wadadisi wa siasa
wanaona kama vile chama hicho sasa kimo katika mgawanyiko mkubwa , kwa
sababu uongozi wa juu haujakaa vizuri. Kila mwalimu na mwelekeo wake, Maalim
Sefu ana mambo yake na Profesa Lipumba anasema hayakubali anayoyasema Maalimu
Sefu.
Profesa Lipumba
anasema yeye ni ngangari kinoma
na ni bado mwenyekiti wa CUF licha ya kuwa alisikia vyombo vya habari
vikitangaza kuwa katibu mkuu Maalim seif amemwondoa katika uenyekiti.
Na Katibu Mkuu, Maalim Seif anaonekana naye yuko imara katika
kutaka kumng’oa Profesa katika nafasi hiyo.Kamweka Mtatiro kuwa Mwenyekiti, mtu
ambaye ni bingwa wa sheria kutoka Chuo Kikuu cha Dar es Salaam.
Chanzo ni kuwa wakati wa uchaguzi mkuu mwaka jana (2015)
baada ya Edward Lowassa kutemwa na Chama cha Mapinduzi, alitaka mahali pa
kujibana ili apate fursa ya kugombea.
(Inasemekana) alikwenda katika vyama vingi, na alipokwenda
kwa Profesa alishauriwa aende Chama Cha Demokrasia (CHADEMA).
Wanasema kuwa Lowassa alitaka kuingia CUF, swali likawa nani
atakuwa mgombea na nani mgombea mwenza?
Kwa katiba ya CUF Lowassa hakuweza kuingia mara moja na kuanza kugombea
nafasi ya kitaifa mara moja kabla hajakaa katika chama cha Wananchi kwa muda wa
miezi sita (6) kwa mujibu wa Katiba.
Lakini kwa Lowassa peke yake
kuwa huko CHADEMA ilionekana kuwa hawezi kupata kura za Waislamu ambao
ni kundi kubwa nchini licha ya kujaribu kwake kuwekeza kwa
kutoa misaada ya kuwasaidia sehemu mbali mbali pamoja na kutoa misaada katika
misikiti kadhaa.
Hivyo, ili kufikia hatua ambayo ingelimweka pazuri na aone
yuko vema ni kumpata Maalim Juma Duni wa CUF aingie CHADEMA kama mgombea mwenza
kwa ajili ya kupata kura za Waislamu.
Kilichomfanya Lowassa akose kupata kura hizo ni kauli ya
Mchungaji ambaye alikuwa mshauri wake wa mambo ya dini huko katika kampeni alipotangaza kuwa Lowassa akitawala, basi
misikiti yote nchini baada ya siku mia moja itageuka na kuwa “nursery schools”
Ilikuwa rahisi kwa Lowassa kuingia CHADEMA , kwanza kama home
boy na nadhani katiba ya chama hicho haina vikwazo kama vya CUF, ndiyo maana
Mwalimu Juma Duni aliweza kuingaia pampja na Lowassa na wote wawili wakafanya
kazi kama majeshi ya kukodi ya CHADEMA. Na mara tu baada ya uchaguzi na
kukosa kilichokuwa kinakusudiwa mgombea
mwenza alirejea zizini CUF.
CUF isingelifanya uchaguzi wa ndani mara baada ya uchaguzi
maana Juma Duni ambaye alikuwa anaaminika kuwa angelikuwa Mwenyekiti baada ya
Profesa kujiuzulu uenyekiti kabla hajafikisha miezi sita kulingana na katiba.
Na mkutano ulioandaliwa hapa Dar es Salaam inasemekna ilikuwa kama kiini
macho maana uliandaliwa visiwani lakini
watu wa Bara hawakukaribishwa. Kwa kawaida Visiwani wajumbe wake huwa ni wachache
kuliko wajumbe wa Bara lakini wajumbe wa
Visiwani safari hii walikuja wengi zaidi ya wajumbe wa bara na wajumbe wengine wa Bara anasema Profesa hawakuwa na habari ya
kikao hicho akiwemo yeye.
Anasema kweli aliomba kujiuzulu uenyekiti kabla ya Uchaguzi
Mkuu mwaka 2015, lakini alitengua hilo kwa barua yake nyingine na kwa hali hiyo
yeye anasema ni Mwenyekiti wa CUF na Msajili wa Vyama nchini analijua hilo.
Asilokubali Lipumba ni
kuwa ametangazwa kuwa si Mwenyekiti kwenye vyombo vya habari , lakini
hajaambiwa rasmi ama kwa simu au kwa barua. Aletewe barua ili aone kimesema
nini na tuhuma zake ni zipi. Anasema mchezo unaofanyika ni kuwa wanataka siku
14 zipite ili asipate fursa ya kufanya rufaa.
Sasa, watu wanasema CUF ni chama cha nani na cha wapi? Kama
cha Visiwani alikianzisha nani? Na kama
cha Bara Mapalala yuko wapi? Kikimeguka kuna faida gani itatokea?
Habari za mbali zinaeleza kuwa Maalim Seif na Profesa Lipumba
walikuwa pamoja katika moja ya taasisi za kielimu hapa nchini katika udogo wao,
na inasemekana wanajuana fika: “Wakiwa kwenye jukwa la siasa wanakaa kama Mr Chairman and Secretary General,
lakini wakiwa nje haisemeki hao watu walivyo karibu. Wanakumbatiana na kuleta jokes
za miaka ya 1970s huko masomoni kwao.
Mwisho/
No comments:
Post a Comment