Monday, September 5, 2016

KUKAMATWA KWA JUA


Dar es salaam
Septemba Mosi ni siku ambayo kwa jiji la Dar es Salaam, licha ya hali ya hewa kuwa na mawingu, maelfu ya watu walishuhudia kupatwa kwa juwa na hali kuwa kama vile  jua japo lipo lakini halina nguvu wala mwanga wake hauna nguvu kama.


                                KUPATWA  KWA JUA MBARALI-MBEYA
Hali hiyo ilisababisha watu kuingiwa hofu na kujiuliza kuna nini kwasababu hali ya kukamatwa jua  au kupatwa kwa mwezi si jambo la kawaida.
Kwa hapa Dar es Salaam mwaka 1976 jua lilipatwa  saa za asubuhi  na mji ukawa umeingia mzizimo, watu waliingia kubishana kwa nini imetokea wengine walisema ni kwa sababu Mohammad Ali – Cacius Clay alikuwa kamtwanga  mangumi mpinzani wake George Foreman huko  Manila – The Manila Chila.
Ama kwa tukio la Septemba Mosi 2016, kilichoonekana ni kuwa Waislamu waliita kwa ajili ya sala na waliingia misikitini na kusali, maelezo ni kuwa, Walikuwa wanatukuza Uungu waMwenyezi Mungu”
“Mwaliona jua lilivyo kuwa na ukali wa joto ulivyo leo licha ya kuwepo  lakinilinaonekana kuwa li baridi” alisikika Imam wa msikiti mmoja hapo Magomeni Mapipa.  Walisimama kuswali mpaka jua lilipo kuwa tena limerudia hali yake ya kawaida na tayari swala ya Adhuhuri ilikuwa imeingia  na watu waliunganisha nakuswali hiyo swala ambayo huiswali kila siku nyakati hizo.
Hali ya kukamatwa jua na kutokea kuwa gubi gumbi kabisa ilitokea Novemba Mosi mwaka 1948. Hizo ni taarifa ambazo ni kwa mujibu wa NASA chombo ambacho ni huko Marekani, ambacho kimejaza mabingwa wa mambo ya anga na hali za hewa. Hao ndio walipeleka timu ya watu kwenda kutua mwezini.
Wakati wa kukamatwa jua unatofautiana  kuna sehemu ambazo ilikuwa ni sehemu kidogo ambapo kivuli cha mwezi kiliangukia ardhini na hiyo ndiyo hali iliyotokea jijini Dar es Salaam. Na sehemu zingine kama kule Njombe hali ilikuwa ni kuwa kufunikwa kabisa; licha ya kuwa ni mchana lakini hakuna jua wala athari yake haikuonekana.
Wakati Waislamu wanasema  wanasimama kuswali kumtukuza Mungu kwa  utukufu wake, kuna taarifa  zinazoeleza kuwa watu wa dini zingine kama wapagani wao walichukua ngoma na kuanza kupiga ngoma zao ili kulitisha lile mzuka lililo gubika jua liondoke na kuliachia jua katika hali yake.
Udadisiwetu haukwenda ndani zaidi, lakini kuna matukio kadhaa yaliyotokea kama kule Sinza  karibu na  mabwalo ya Lulu na Utoji kuna madibwi ya maji  na  vijana walizunguka madimbwi hayo na kuangalia hali hiyo, wanasema kwa kutumia kivuli cha jua ndani ya maji haina athari kwa macho kama mtu akiangalia  moja kwa moja angani.
Watu wengine  ambao walikuwa karibu na mafundi wa welding, walitumia kile kioo ambacho hutumika kwa kuchomelea vyuma, na ikawa ni deal ya kukodishwa watu kwa  dakika moja moja na  yulemtu aliyesimamia zoezi hilo inasemekana kaondoka na kiasi cha mboga. Kila kichwa(mtu) ilikuwa shilingi mia mbili (200/=)
Katika kituo kimoja cha  mabazi  sehemu ya mapipa, walisikika, watu wakisema kuwa je hali hiyo  wanasayansi hawawezi kuingilia kati na kuizuwia ili  kupunguza hofu kwa watu?
“Ah Bwana  wana Sayansi wanasoma hali ya kitu kilivyo na wanaweza kujaribu kuelezea tu lakini  wajaribu kuepusha jua lisipatwe na mwezi au mwezi usipatwe na jua, hajatokea mbishi wanamna hiyo na hatatokea mpaka mwisho wa dunia!
Lakini yule mdadisi aliendelea kusema mbona wamepiga hatua mpaka wameumba  kondoo wao wenyewe  na hivi sasa wanaweza kuunda mimba nje ya mimba na kuiitia tumboni mwa mwanamke  ambaye ni mgumba?”
“Astaghfirullahi! Enhe ndio wamefika kuumba ili nao waabudiwe?  Sikiliza  bwana Hakuna anaweza kuunda manii wala yai la mwanamke  jinsi vilivyo hivi vitu watachukua na kujaribu tu, lakini Hakuna uunga wala uunmbaji wamwogope Mola wao. Firauni alidai kuwa yu Mungu na kusema alikuwa anapitisha mito naalikuwa ana mabustani nchini kwake … na yalimfika yaliyo mfika  maji hayo hayo aliyokuwa anajifanya Ndiyo neema zake yalimwangamiza alipojaribu kumfuata Musa ili amwuue. Bwana we wanaweza kujaribu kutabiri lini hayo yatatokea lakini kuyazuwiya ni Ng’odo!”

PICHA ZIFUATAZO ZINAONYESHA KUPATWA KWA JUA MBARALI-MBEYA


WATU WAKIANGALIA KUPATWA KWA JUA KUPITIA KIFAA MAALUMU






No comments:

Post a Comment